Tuesday, November 15, 2016

MASHINDANO YA MISS TANZANIA KUBORESHWA.

Image result for MISS TANZANIA
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amesema Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha mashindano ya ulimbwende yanakuwa na thamani na yenye faida.
Nape aliyasema hayo wakati akimkabidhi bendera ya Taifa, Miss Ilala 2016, Julitha Kabete ambaye pia ni mshiriki wa mashindano ya Miss Tanzania 2016, ambaye anakwenda kushiriki mashindano ya urembo Afrika yatakayofanyika Novemba 26 katika kitongoji cha Calabar nchini Nigeria.
“Tunataka mashindano ya Miss Tanzania ambaye anafaidika sio mshindi peke yake tumeona hapa huyu alikuwa mshindi wa nne na amepata nafasi ya kuwakilisha nchi, tunafahamu mashindano ya Miss Tanzania yalikuwa yamefungiwa kufanyika ila sasa yamerudi vizuri, tutaendelea kuyaimarisha yawe bora na matarajio ya serikali ni kuona tunakuwa tunafanya vizuri na siku moja hata mshindi wa Miss World atoke Tanzania,” alisema Nape.
Pia Nape alisema serikali inamtakia safari njema na ipo nyuma yake kumpa msaada pindi unapohitajika.
Akizungumza wakati wa kukabidhiwa Miss Julitha Kabete amesema amejiandaa kwa ajili ya mashindano hayo na anaamini atafanya vizuri kwenye mashindano hayo ambayo ndio kwanza yanaanza.
“Naomba Watanzania wanisapoti ili nifanikiwe kushinda Miss Africa ambayo inafanyika Nigeria, ni nafasi ya kipekee ambayo nimepata na nikipata ushindi ni wetu sote,” alisema Julitha.
Mashindano hayo yatafanyika kwa mara ya kwanza Afrika katika kitongoji cha Calabar kilichopo Nigeria. Naye mrembo huyo akizungumza katika hafla hiyo alisema kuwa amejiandaa vizuri kwa ajili ya shindano hilo la kwanza kufanyika.

WAHITIMU WA ELIMU YA JUU KUBANWA.

mtz1
Sheria mpya ya kulipa mikopo kwa wahitimu wa elimu ya juu iliyopitishwa na Bunge hivi karibuni, itazidisha machungu kwa waajiriwa wapya na wale wa zamani.
Kwa mujibu wa sheria hiyo, wakopaji hao wataanza kukatwa deni hilo moja kwa moja kutoka kwenye mishahara yao baada ya mwaka miaka miwili tangu walipomaliza masomo yao.
Kwa mujibu wa sheria hiyo, wakopaji ambao tayari wamehitimu na kuajiriwa watakutana na kibano katika kulipa deni hilo kwa kukatwa asilimia 15 ya mshahara wao.
Mbali ya makato hayo, mtumishi mpya ambaye ataajiriwa baada ya kumaliza masomo yake,   mshahara wake pia itabidi ukatwe kodi ya mapato (Payee) pamoja na makato mengine yakiwamo ya mifuko ya jamii, chama cha wafanyakazi na bima ya afya.
Mathalani, muhitimu wa Shahada ya kwanza ya udaktari ambaye kwa mujibu wa sheria anapokea mshahara wa Sh 1,480,000, baada ya makato atabakiwa na wastani wa Sh 754,300.
Katika mchanganuo huo, mwajiriwa  atakatwa asilimia 15 kodi ya mapato, sawa na Sh 326,000, Sh 148,000 ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), deni la mkopo  wa HESLB Sh 222,000.
Katika orodha hiyo, pia kuna makato ya    Sh 29,600 ya chama cha wafanyakazi mbali na makato ya Bima ya Afya ambayo mfanyakazi hukatwa kulingana na mshahara wake.
Watumishi wengine watakaokumbana na panga hilo la makato ni   walimu na wauguzi ambao wamenufaika au watanufaika na mkopo huo wa Serikali.
Kwa mwalimu mwenye Shahada ambaye mshahara wake unaanzia Sh 716,000 atalazimika kubaki na Sh 565,500 huku mwenye Stashahada   ambaye mshahara wake wa kuanzia ni Sh 530,000 atabakiwa na wastani wa Sh 440,000 baada ya makato yote, kwa mujibu wa sheria.
Wakati huohuo, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) jana ilitangaza kuwasaka kwa udi na uvumba wadaiwa wote sugu 142,470 ili wafikishwe mahakamani.
Wadaiwa hao ni walionufaika na mkopo  tangu mwaka 1994-1995 hadi Juni mwaka huu na kufikisha deni la zaidi ya Sh 239,353,750,176. 27.
Ili kuhakikisha fedha hizo za mikopo zinapatikana, HESLB itawasilisha majina ya wadaiwa hao kwenye taasisi za fedha ili kutathmni tabia zao kabla ya kukopeshwa au kuwadhamini.
Akizungumza   Dar es Saalam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul- Razaq Badru alisema kuanzia sasa wadaiwa hao na wadhamini wao wanapaswa wajisalimishe kwa bodi hiyo vinginevyo watafikishwa mahakamani.
“HESLB inatoa notisi ya siku 30 kwa wadaiwa hao  walipe kiasi chote cha madeni yao baada hapo watafikishwa mahakamani.
Hata hivyo, alisema Sh 51,103,685,914 ni deni lililorithiwa kutoka kwa iliyokuwa Wizara ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia ambazo zilizokopeshwa kwa wanafunzi 48,378 tangu mwaka 1994 hadi Juni mwaka 2005.
Badru alisema kuanzia Julai, mwaka 2005 hadi Juni 30, mwaka huu Bodi imetoa Sh 2,544,829,218,662.50 kwa wanafunzi 330,801.
Hali hiyo inafanya  jumla ya fedha zilizokopeshwa tangu mwaka 1994/95 hadi 2015/2016 kufikia Sh 2,595,932,575.56 ambako wanafunzi 379, 179 wamenufaika nazo.
Badru alisema kati ya mikopo yote iliyotolewa kuanzia mwaka 1994/95 mpaka Juni mwaka huu, mikopo iliyoiva ni Sh 1,425,782,250,734.31 ambayo ilitolewa kwa wanufaika 238,430.
Mkurugenzi Msaadizi wa Mikopo kutoka HESLB, Dk. Abdul Mussa Ally alisema hali ya urejeshaji wa mikopo ni nzuri.
Alisema  katika   mwaka wa fedha uliopita, Sh bilioni 36 zimekusanywa na Julai hadi Oktoba mwaka huu zimekusanya Sh bilioni 25,000.
Ally alisema ukusanyaji wa fedha hizo  umezidi kuongezeka  kutoka  Sh bilioni mbili  kwa mwezi hadi Sh bilioni sita hadi saba kwa mwezi hivi sasa.

WANAOSHINDANIA TUZO YA BBC YA MWANAKANDANDA BORA AFRIKA 2016.

Piga kura sasa
Wachezaji watano watakaoshindania Tuzo ya BBC ya Mwanakandanda Bora wa Afrika wa Mwaka 2016 wametangazwa.
Wachezaji hao ni;
Pierre-Emerick Aubameyang
Andre Ayew
Riyad Mahrez
Sadio Mane
Yaya Toure.
Wachezaji hao watano walitangazwa wakati wa kipindi maalum cha moja kwa moja runingani Jumamosi.
Piga kura hapa : bbc.com/africanfootball
Mshindi atachaguliwa na mashabiki wa soka ya Afrika kutoka kila kona ya dunia. Mashabiki wana hadi saa 18:00 GMT tarehe 28 Novemba kumpigia kura mchezaji wanayempenda.
Mnamo Jumatatu, 12 Desemba, mshindi wa tuzo hiyo atatangazwa moja kwa moja kwenye runinga ya BBC Focus on Africa pamoja na redio, kuanzia saa 17:35.
Tovuti za BBC SwahiliBBC Sport na BBC Africa pia zitachapisha habari za mshindi.
Aubameyang ameorodheshwa kwa mwaka wanne mtawalia, mshindi wa mwaka 2011 pia ameorodheshwa kwa mwaka wa nne, Mahrez ndiye mchezaji pekee ambaye hajawahi kuorodheshwa kushindania, Mane alishindania mara ya kwanza mwaka jana naye mshindi mara mbili. Toure ameorodheshwa kwa mwaka wa nane mtawalia.

WANANCHI WAIPINGA SERIKALI KUTUMIA FEDHA ZA MAAFA YA TETEMEKO.


Msimamo wa Serikali wa kutumia michango iliyotolewa kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera kujengea miundombinu umeendelea kupingwa, huku baadhi ya wananchi na wanasiasa wakitaka suala hilo liangaliwe upya.
Diwani wa Kashai (Chadema), Nuruhulda Kabaju akizungumza kwa kile alichodai kuwa ndiyo maoni ya wananchi, alisema wahisani waliotoa misaada walilenga kuwasaidia kwanza wananchi na suala la kujenga majengo ya Serikali lingefuata baadaye.
Kwa mujibu wa diwani huyo, kata hiyo imesajili nyumba 636 zilizobomoka na kaya 2,556 kukosa makazi na kati ya hizo, Shirika la World Vision Tanzania limetoa mifuko 212 ya saruji na nyumba 1,300 ni hatari kuishi.

KIDATO CHA PILI WAANZA MITIHANI YA TAIFA.

CHARLES MSONDE.
Jumla ya watahiniwa 435,221 wamesajiliwa kufanya upimaji wa Kitaifa wa Kidato cha Pili huku watahiniwa 1,045,999 wakisajiliwa kwa ajili ya Darasa la Nne kwa mwaka huu.
Upimaji wa Kidato cha Pili umeanza jana hadi Novemba 25 katika shule za sekondari 4,669 wakati ule wa Darasa la Nne utafanyika Novemba 23 na 24 katika shule za msingi 17,032 Tanzania Bara.
Akizungumzia upimaji wa Kitaifa wa Kidato cha Pili, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Dk Charles Msonde alisema idadi hiyo ni ongezeko la watahiniwa 38,451 ambayo ni asilimia 9.7 ya watahiniwa 396,770 waliosajiliwa mwaka 2015.
Dk Msonde alisema kati ya watahiniwa waliosajiliwa wavulana ni 214,013 sawa na asilimia 49.17 na wasichana ni 221,208 ambao ni asilimia 50.83 huku watahiniwa 67 ni wasioona na 306 wenye uoni hafifu.
Matokeo ya Kidato cha Pili mwaka 2015, yanaonesha kuwa wanafunzi 324,068 ambao ni sawa na asilimia 89 kati ya wanafunzi 363,666 waliofanya mtihani walifaulu na kuendelea na kidato cha tatu.
Kwa upande wa upimaji wa Kitaifa wa Darasa la Nne, Dk Msonde alisema kati ya waliosajiliwa wavulana ni 507,732 sawa na asilimia 48.54 na wasichana ni 538,267 ambao ni asilimia 51.46 huku watahiniwa 76 ni wasioona na 483 kwenye uoni hafifu.
“Katika upimaji wa kitaifa wa mwaka huu kumekuwa na ongezeko la watahiniwa 8,694 ambao ni asilimia 0.8 ukilinganisha na watahiniwa 1,037,305 waliosajiliwa mwaka 2015,” alisema.
Matokeo ya Upimaji wa Darasa la Nne 2015 yanaonesha kuwa wanafunzi 869,057 kati ya wanafunzi 977,886 sawa na asilimia 88.87 waliofanya upimaji wamepata alama katika madaraja ya A,B,C na D huku wanafunzi 108,829 sawa na asilimia 11.13 wamepata alama za ufaulu usioridhisha.
“Maandalizi yote kwa ajili ya upimaji huo yamekamilika, ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa mitihani na nyaraka zote muhimu katika mikoa na halmashauri zote za Tanzania Bara,” alisema na kuongeza kuwa upimaji wa Kidato cha Pili ni muhimu kwa wanafunzi ili kupima uwezo wa uelewa wa wanafunzi katika yale waliyojifunza kwa kipindi cha miaka mwili ya masomo na kwa Darasa la Nne ni kujua kiwango cha wanafunzi kumudu stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu.
Aidha, Msonde amezitaka Kamati za Mitihani za Mikoa na halmashauri au manispaa kuhakikisha kuwa taratibu za upimaji zinazingatiwa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mazingira ya vituo yapo salama, tulivu na kuzuia mianya ya udanganyifu na kwamba Baraza litachukua hatua kali kwa yeyote atakayebainika kukiuka taratibu za uendeshaji wa upimaji wa Kitaifa.

Saturday, November 12, 2016

SITTA APUMZISHWA KWENYE NYUMBA YAKE YA MILELE HUKO TABORA.

Mamia ya wananchi mkoani Tabora wamejitokeza kumuaga Spika wa Bunge Mstaafu, Samuel Sitta aliyefariki usiku wa kuamkia Jumatatu ya wiki hii.
Wananchi hao wamejitokeza katika Uwanja Shule ya Msingi Urambo jirani ya nyumbani kwake Sitta shughuli ya kutoa heshima za mwisho wa wananchi hao imeanza saa moja asubuhi.
Wananchi hao walijipanga katika mstari mrefu kwa ajili ya kupita pembeni ya jeneza lenye mwili wa Sitta, ambapo toka asubuhi maduka mengi wilayani Urambo yalikuwa yamefungwa.

BARAKA DA PRINCE ANAHITAJI MSAADA.

barakah-1-656x800
BARAKA NA NAJ
Mtoto wa miaka miwili badala ya kusema kikombe akatoa tusi, hufai kumpiga wala kumgombeza. Unachotakiwa kufanya ni kumtia nguvu katika juhudi zake za kujifunza na kumwambia kwa usahihi neno kikombe linavyotamkwa. Hivyo ndivyo hata kwa mtu mgeni katika miji mikubwa.
Mshamba akitoa huko mashambani na kukutana na lifti  katika majengo makubwa na kutaka kuvua viatu kisha ndio aingie, ukimcheka utakuwa juha.
Sasa unamcheka nini na hayo mambo kwao hakuna? Unashanga kitu gani yeye kuvua viatu na kutaka kuingia katika lifti wakati huko kwao kafundishwa ni ustaarabu ukikuta maeneo nadhifu uvue viatu?
Nimetoa mifano hiyo nikikumbuka tabia ya msanii Baraka Da Prince. Kwa siku za hivi karibuni bwana mdogo amekuwa na matukio na kauli za ajabu na cha kushangaza watu wanamshangaa na wengine kumtolea maneno makali.
Ni kweli Baraka anafanya mambo ya kijinga, yasiyofaa kufanywa na mtu anayejitambua. Ila mimi sishangai hayo mambo kufanywa na mtu aina ya Baraka.
Yangefanywa na Diamond, Ali Kiba na akina Chegge  ningeshangaa mno. Nishangae vipi Baraka kuposti nyumba ya mama yake Naj na kusema ni yake wakati najua kijana wetu huyu bado hajatokwa matongotongo machoni?
Katu siwezi kushangaa na yeyote atakayemshangaa, nitamshangaa yeye. Ni jambo linalotarajiwa kabisa kwa kijana ambaye miaka mitatu nyuma alikuwa akishindia kababu na mihogo huku akiwa ndani ya kaptura chafu isiyojulikana rangi yake, viatu vilivyotoboka na akiwa anadhihakiwa na kila msichana anayejaribu kumchombeza, kuwafanyia unyama ndugu zake kisa kuwa na msanii Naj katika mapenzi.
Baraka ni kwanini asitokwe na akili kwa Naj wakati miaka mitatu iliyopita alikuwa akimuona bibie katika magazeti na majarida akiwa kakumbatiwa na Mr Blue, msanii ambaye Baraka huyu amekuwa akimuona toka kipindi anaomba Shilingi ishirini akanunue ice cream kwa mama John?
Siwezi kumlaumu Baraka. Kumlaumu Baraka kwa ujinga anaoufanya ni sawa na kulaumu mtoto mdogo anapotukana kipindi akijifunza kuongea.
Siku moja katika mitandao ya kijamii Baraka baada ya kuposti picha ya mpenzi wake, Najma Dustan, msanii mwenzake, mtoto wa mjini Msami akamtania kwa kujifanya anamtamani Naj.
Kilichotokea kiliniacha hoi kwa kicheko. Baraka akatokwa na matusi kwa Msami na kumwambia akamtamani dada yake.
Baraka anatupa maneno haya kwa mtu ambaye amekuwa akionekana katika video na magazeti kwa zaidi ya miaka sita sasa.
Anatokwa povu la kijinga kwa Msami kwa kudhani kuwa eti ni kweli anamtamani mpenzi wake huku akiwa amesahau ni Msami huyu ambaye aliwahi kudaiwa kutoka na mastaa wengine wakubwa wa Bongo.
Msami ni mtoto wa  mjini sana kuliko Baraka. Msami kaona mengi ya kimjini kuliko yeye. Kutoka  dansa hadi kuwa msanii mwenye kueleweka, Baraka anatakiwa ajue uzito wa Msami.
Yeye bado ni mgeni katika jumba la mastaa, anayofanya ni sehemu ya ulimbukeni wa kawaida kwa mgeni. Kumlaumu au kumkosoa sana ni kumkosea.
Anayofanya Baraka ni sawa na mtu ambaye hajawahi kumiliki au kuendesha gari zuri la thamani. Atatembea kila eneo kutaka kuonesha kuwa anaendesha gari zuri. Huu ni  ulimbukeni.