Thursday, November 24, 2016

INSTAGRAM YAZINDUA VIDEO YA MATANGAZO YA MOJA KWA MOJA.

Video ya matangazo ya moja kwa moja ya Instagram
Mtandao wa Instagram ndio mtandao wa huduma ya kijamii wa hivi karibuni kuzindua video za matangazo ya moja kwa moja.
Ukifuata nyayo za mtandao wa facebook,unaomiliki Instagram,You Tube pamoja na programu ya moja kwa moja ya Twitter ya Periscope ,Instagram imezindua programu mpya inayoruhusu wateja wake kuweka matangazo ya moja kwa moja wakati wowote.
Mtu yeyote anayetazama anaweza kutoa maoni yake kwa kuweka emoji ambazo hujitokeza katika video hiyo ya moja kwa moja.
Inaonekana kuwa ya kawaida,lakini kuna tofauti kubwa.Mara tu unapomaliza kuweka matangazo yako hupotea kabisa.
Hiyo inamaanisha hutaweza tena kusambaza link ya video yako kwa wanaotazama na hawataweza kuiona tena baada ya matangazo hayo.
Katika taarifa, msemaji wa Instagram alisema kuwa hiyo inalenga kuwafanya wateja kuhisi faraja na kuweza kusambaza chochote wanachotaka kusambaza.
Programu hiyo itasambazwa kwa kundi la wateja wa mtandao huo kabla ya kutumika na kila mtu katika kipindi cha wiki chache zijazo.

JUSTIN BIEBER AONEKANA AKIMPIGA NGUMI SHABIKI.

Image result for JUSTIN BIEBER
JUSTIN BIEBER.
Bado mwanamziki Bieber anaendelea na mikasa yake ya kupigana hadharani. Kanda ya video inayomuonesha Justin Bieber akimpiga ngumi shabiki wake usoni imetolewa.
Mtu huyo anaonekana kupeleka mkono wake katika dirisha la gari ya Bieber ambapo anapigwa ngumi na kuachwa akitoka damu mdomoni.
Kanda hiyo inaonekana kurekodiwa mjini Barcelona,ambapo msanii huyo alikuwa akitumbuiza ikiwa ni miongoni mwa ziara yake ya muziki.
Gari moja linaendeshwa polepole katika umati wa watu na msani huyo wa miaka 22 anaonekana kuwa katika kiti cha nyuma huku kioo chake cha dirisha la gari kikiwa wazi.
Shabiki huyo anaonekana kuingiza mkono katika dirisha la gari hilo na kujaribu kumshika Bieber.Wakati gari linapoondoka mkono unaonekana ukitoka katika dirisha hilo.
Shabiki huyo baadaye anarudi nyuma na kuisogelea kamera akiwa na damu katika meno yake na midomo.
Newsbeat imewasiliana na wawakilishi wa msanii huyo lakini haijapata tamko lolote kutoka kwao.
Mapema siku hiyo msanii huyo alipigwa picha akifanya zoezi na wachezaji wa Barcelona.

AL QAEDA YATHIBITISHA KUUAWA KWA KIONGOZI WAO MKUBWA.

Ndege za kivita za Marekani zilimlenga al-Qahtani katika mji wa Kunar
Kundi la kigaidi la Al-Qaeda limethibitisha kuuawa kwa kiongozi wao mkubwa Farouq al-Qahtani huko kaskazini Mashariki mwa Afghanistan katika mapigano na vikosi vya marekani mwezi mmoja uliopita.
Huko mjini Washington wamethibitisha kifo hicho kutokea November 15 yalikuwa ni makabiliano adhimu.
Lakini Al-Qaeda wamesema kuwa mkewe na watoto waliuwawa pia japo hawakujulikana kijeshi.
Vikosi vya Marekani vimeiweka Al-Qahtani mzaliwa wa Saudi huko Quatar kama mtu wanayemtafuta sana kwao akituhumiwa kuhusika na mipango ya mashambulizi huko Marekani na Ulaya.

MATUKIO KATIKA TUZO ZA AMAs HUKO MAREKANI.

rihanna
RIHANNA.
Wavunja rekodi
Wakali wa muziki wa Pop kutoka Canada, Aubrey Drake na Justine Bieber wamevunja rekodi ya aliyekuwa mfalme wa muziki wa pop duniani, Michael Jackson, baada ya kunyakua tuzo nne kila mmoja katika tuzo hizo.
Drake amenyakua tuzo ya msanii bora wa mwaka, msanii wa hip hop anayependwa, albamu ya hip hop inayopendwa ‘Views’, wimbo wa hip hop unaopendwa ‘Hotline bling’.
Beiber amenyakua tuzo ya video bora ya mwaka ‘Sorry’, msanii wa kiume wa muziki wa Pop anayependwa, albamu inayopendwa zaidi ya Pop ‘Purpose’ na wimbo unaopendwa wa Pop ‘Love Yourself’.
Licha ya kunyakua tuzo hizo nne, jina la Drake kwa mara ya kwanza lilikuwa katika vipengele 13, lakini akanyakua tuzo nne na Bieber naye alikuwa akiwania tuzo sita akanyakua nne.
Tangu tuzo hizo zilipoanza mwaka 1972, Michael Jackson ndiye msanii pekee aliyeweka historia ya jina lake kuwa katika vipengele 11 mwaka 1984 hadi Drake alipoivunja rekodi hiyo mwaka huu kwa kuwa katika vipengele 13.
Hata hivyo, Drake aliwataka mashabiki wake kutumia jina lake vizuri, huku akijinadi kuwapoteza kimuziki wasanii wenye majina makubwa zaidi yake.
Rihanna
Mkali wa muziki wa RnB, Robyn Rihanna Fenty ‘Rihanna’ alifuata kwa idadi kubwa ya tuzo baada ya kujinyakulia tuzo tatu, huku Twenty One Pilots nao wakinyakua tuzo mbili.
Rihanna amenyakua tuzo ya wimbo bora unaopendwa wa RnB ‘Work’, albamu ya RnB inayopendwa ‘Anti’ na msanii wa kike wa RnB anayependwa.
Walionogesha
Wasanii wengine ambao waliwagusa mashabiki kutokana na shoo kali ni pamoja na John Legend kutokana na wimbo wake wa ‘Love Me Now’, wengine ni Ariana Grande na Nicki Minaj, ambao walipiga shoo ya kuvutia.

MENEJA WA LADY JAYDEE AZUNGUMZIA KUHUSU TETESI ZA NDOA ZA JIDE.

jde
LADY JAYDEE NA MUMEWE.
Kufuatia sintofahamu kwa mashabiki wake kuhusiana na tetesi za kufunga ndoa na kwenda mapumziko visiwani Zanzibar, mwanamuziki, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ anatarajia kuweka wazi suala hilo hivi karibuni.
Akizungumza jana, Meneja wa mwanamuziki huyo, Seven Mosha, hakutaka kuzungumzia suala hilo, huku akisisitiza kwamba Lady Jaydee mwenyewe ataliweka wazi suala hilo hivi karibuni.
“Habari hizo zipo kwenye mitandao, lakini suala hili anatakiwa kuliongelea mhusika mwenyewe, mimi sina la kuzungumza, ni mapenzi yake ila naamini ataliweka wazi mwenyewe suala hilo hivi karibuni,’’ alieleza Seven.

PANYA BUKU KUPIMA SAMPULI ZA UGONJWA WA KIFUA KIKUU (TB).

Mkurugenzi wa Uhakiki Ubora wa Huduma za Afya, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Mohamed Ally Mohamed (kushoto) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kituo cha ugunduzi wa Kifua Kikuu kwa kupitia panya buku (Apopo) kilichopo Dar es Salaam. Wengine ni Mwalimu wa panya, Ezekiel Mwakyonde (aliyemshika panya) na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Dk Abdu Hayghaimo. Sherehe hizo zilifanyika jana. (Picha na Yusuf Badi).
Maabara ya kupima sampuli za ugonjwa wa kifua kikuu (TB) kwa kutumia panya buku wa Mradi wa Apopo ulio chini ya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), imezinduliwa jijini Dar es Salaam, huku ikielezwa kuwa panya mmoja ana uwezo wa kupima sampuli 100 ndani ya dakika 20.
Uzinduzi wa maabara hiyo ulifanywa jana na Mkurugenzi wa Uhakiki Ubora wa Huduma za Afya wa Wizara ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Mohamed Mohamed kwa niaba ya waziri wa wizara hiyo na uzinduzi ulioshuhudiwa na wadau mbalimbali pamoja na wananchi.
Akielezea mradi huo wa kupima vimelea vya kifua kikuu kwa kutumia panya waliofunzwa, Meneja Mradi, Dk Georgies Mgode alisema panya hao wana uwezo wa kubaini harufu ya vimelea vya ugonjwa huo ndani ya sekunde.
Aidha, alisema kwa dakika 20 panya anaweza kupima sampuli 100 wakati sampuli kama hizo zingepimwa kawaida kwenye maabara zinazotumia hadubini kwa siku nne, hivyo majibu hadi yafike kwa mgonjwa yanaweza kuchukua siku saba ili hali kwa kutumia panya mgonjwa ndani ya siku moja anapata majibu na kuanza tiba.
“Ni kweli hawa panya wana faida kubwa kwenye ugunduzi wa vimelea vya ugonjwa wa TB, kwa sababu wana uwezo ndani ya sekunde wakabaini maambukizi ya kwa mgonjwa wakati mtu wa maabara anatumia zaidi ya siku moja kupata majibu,” alisema Dk Mgode.
Alisema kwa kuzinduliwa kwa maabara hiyo itakayokuwa na panya buku 10 jijini Dar es Salaam ni hatua ya mafanikio ya harakati za vita dhidi ya ugonjwa huo hasa kwa kuwa jiji hilo ndilo linaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watu, kuliko maeneo mengine na pia ni moja la miji yenye idadi kubwa ya wagonjwa wa kikua kikuu.

WIMBO WA RICH MAVOKO NA DIAMOND "KOKORO" KUCHUNGUZWA.

screenshot-from-2016-07-01-134855
DIAMOND PLATNUMZ.
Video ya wimbo mpya wa ‘Kokoro’ ulioimbwa na wasanii wa Bongo Fleva kutoka kundi la Wasafi, Richard Martin (Rich Mavoko) na Nassib Abdul (Diamond Platnumz), unachunguzwa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Bodi ya Filamu na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kama video hiyo ina udhalilishaji wa mwanamke au la.
Mkuu wa matukio wa Baraza hilo, Kurwijira Maregesi, amesema kwamba wanafanyia uhakiki wa video hiyo kutokana na baadhi ya vipande katika video hiyo kuonyesha udhalilishaji wa mwanamke, tabia ambayo inapingwa vikali na jamii.
“Katika kusimamia maadili ya sanaa na udhalilishaji wa wanawake, tuko thabiti kuhakikisha hakuna msanii anayepotosha taifa wala kumdhalilisha mtu,” alisema Maregesi
Maregesi aliongeza kwamba kumekuwa na tabia kwa wasanii wa Bongo fleva kutoa nyimbo zenye kupotosha Taifa.