Saturday, January 14, 2017

WHATSAPP KUJA NA UWEZO WA KUWAWEZESHA WATUMIAJI KUFUTA UJUMBE KABLA YA KUMFIKIA MUHUSIKA.


WhatsApp-4-840x561

Mtandao maarufu wa kijamii WhatsApp upo katika harakati za kuwawezesha watumiaji wake kufuta ujumbe uliotumwa kabla haujapokewa upande wa pili. 

Kuna wakati unaweza kutuma ujumbe fulani kwa bahati mbaya na kugundua umefanya kosa katika WhatsApp, lakini ukashindwa kuufuta kwa sababu tayari umeshatumwa na kupokewa.
Lakini kwa sasa WhatsApp imekuja na wazo la kurekebisha tukio kama hilo kwenye simu zenye mfumo endeshi wa iOS.

Katika hilo kutakuwa na program katika eneo la ‘Settings’, ambapo utatakiwa kue-‘Edit’ kisha ‘Revoke’ mchakato utakaowezesha kufuta ujumbe huo kwa wakati mara tu unapogundua umekosea.
Hata hivyo, kikubwa ni kuwa utaweza kufanya hivyo kama tu uliomfikia bado hajausoma, ikimaanisha iwapo ameshausoma hutaweza kuufuta.

Lakini hadi sasa WhatsApp hawajatoa taarifa rasmi ya lini uwezo huo utaanza kutumika.

Monday, January 2, 2017

DARASA AFUNGA MWAKA KWA KISHINDO NA MUZIKI.

Tumezoea kusikia nyimbo za mapenzi zikipendwa zaidi kuliko zile zenye ujumbe wa masuala mengine muhimu kwa jamii. Mara nyingi ngoma zenye meseji ni zile zinazohusisha mtindo wa kofokafoka yaani Rap.
Kwenye historia ya Bongo Fleva, nyimbo za Rap hazikuwahi kuzizidi zile za mapenzi. Ngoma zenye jumbe za mapenzi zinapendwa zaidi sokoni na ndiyo  zinazochezwa zaidi.
Sasa inakuwaje pale ambapo rapa anavunja rekodi nyingi kwa wakati mmoja ambazo kwa miaka mingi marapa wengine wameshindwa kuzivunja?
Hapo ndipo Swaggaz linapomkumbuka Ramadhan Sharif  ‘Darassa’ ambaye ni bosi wa Lebo ya Classic Music Group (CMG), ambaye anafunga mwaka kwa historia ya aina yake akiwa na ‘Wimbo wa Taifa’ Muziki.
Mwaka ulipoanza Darassa alitupa karata yake ya kwanza kupitia Kama Utanipenda, aliyomshirikisha Rich Mavoko.
Juni 30, akakutana na waandishi wa habari kutambulisha lebo yake ya CMG, staili yake ya kucheza anayoiita Zombie Walk na kuwaweka tayari mashabiki kwa Too Much, wimbo uliotoka Julai 12.
Grafu ya muziki wa Darassa ilizidi kupanda Novemba 23, alipotambulisha ngoma yake mpya, Muziki. Wimbo unaokua siku baada ya siku – wimbo ulioibua vituko mtaani na kupenya mpaka kwa viongozi wakubwa wa Serikali.
Hii ndiyo ngoma yenye mzunguko mkubwa kwa sasa kwenye redio, runinga mpaka kitaa. Usipousikia kwenye nyumba/chumba cha jirani yako basi utausikia kwenye baa iliyo karibu na wewe.
Ni ngumu kuukwepa labla uwe na matatizo ya usikivu ingawa utauona kwenye runinga hata ukiwa una uono hafifu basi utausikia kwenye Bajaj na bodaboda hapo mtaani.


Thursday, November 24, 2016

BIFU LA OMMY DIMPOZ NA DIAMOND LAPAMBA MOTO.

Image result for ommy dimpoz NA DIAMOND
OMMY DIMPOZ NA DIAMOND.
Wiki hii kumekuwa na majibizano kati ya wasanii wakubwa wawili hapa Bongo, nawazungumzia OMMY DIMPOZ na DIAMOND PLATNUMZ.

Hayo majibizano yamekuja baada ya Ommy Dimpoz kupost ujumbe Instagram uliokuwa ukisema kuwa kuna baadhi ya wasanii wamekuwa wakinunua viewers youtube ili video zao zionekane kuwa zinaangaliwa na watu wengi.

Kutokana na ujumbe huo, mashabiki wa Diamond walikuja juu na kuanza kumtukana Ommy, kitu ambacho kilipelekea Diamond naye kujibu ujumbe huo kwenye akaunti yake Instagram.

Hatimaye Diamond akafanya interview na XXL Clouds FM na kutokwa na mapovu juu ya Ommy. Na Ommy pia akatuma ujumbe kuomba kufanya interview XXL naye ili aeleze ya moyoni baada ya Diamond kusema anapumuliwa.

Hili bifu kati ya hawa wasanii wawili linapamba moto na hakuna dalili ya kulizima kiurahisi.

MAAJABU:MWANAMKE AWAPIGA RISASI WAGENI WALIOMTEMBELEA KWA SABABU YA KUPIGA KELELE.

Alana Annette Savell
Mwanamke mmoja katika jimbo la Florida nchini Marekani, aliwafyatulia risasi wageni waliokuwa wamemtembelea kwa sababu walikuwa wamekaa sana na walikuwa wanapiga kelele, polisi wanasema.
Alana Annette Savell, 32, alikuwa mwenyeji wa wageni hao wawili, wapenzi, katika jiji la Panama pale walipoanza kupiga kelele sana.
Polisi wanasema aliwaamrisha kuondoka kutoka nyumbani kwake, kabla ya kuwapiga risasi miguuni.
Walijipeleka hospitalini wakiwa na majeraha, ambayo hayakuwa mabaya sana.
Bi Savell ameshtakwia kwa kuwashambulia watu akitumia bunduki.
Ofisi ya Mwendesha mashtaka wa wilaya ya Bay iliambia BBC kwamba mwanamke huyo kwa jina Kristy Jo Mohr alikuwa amefika na mpenzi wake, ambaye walikuwa wamekutana kwenye baa, nyumbani kwa mshtakiwa mwendo wa saa saba usiku Jumatatu.
Bi Savell aliambia polisi alianza kukerwa na wageni hao baada yao kuanza kunywa pombe na kuzungumza kwa sauti ya juu.
Badala ya kuwadokezea kwamba alikuwa amechoshwa nao kwa kula miayo au kuweka vyombo vya jikoni kwenye mashine ya kuosha vyombo, alichomoa bunduki yake na kuwafyatulia risasi miguuni.
Bi Mohr aliumizwa miguu yote miwili naye mpenzi wake, aliyetambuliwa tu kwa jina Cowboy akaumia mguu mmoja.
Bi Mohr ameambia polisi anakadiria kwamba kwa jumla Bi Savell alifyatua risasi nane au tisa.
Aliposhtukia amepigwa risasi mguuni, anasema alikimbia na kuingia kwenye gari.
Mpenzi wa washukiwa ameambia maafisa wanaochunguza kisa hicho kwamba alikuwa amemshauri kwamba mgeni akikatalia nyumbani baada ya kumwambia mara tatu, achukue bunduki na kufyatua risasi sakafuni.
"Hilo lisipofanya kazi, basi awafyatulie risasi miguuni," maafisa wa mashtaka wamesema.
Bi Savell kwa sasa bado anazuiliwa uchunguzi zaidi ukiendelea.

INSTAGRAM YAZINDUA VIDEO YA MATANGAZO YA MOJA KWA MOJA.

Video ya matangazo ya moja kwa moja ya Instagram
Mtandao wa Instagram ndio mtandao wa huduma ya kijamii wa hivi karibuni kuzindua video za matangazo ya moja kwa moja.
Ukifuata nyayo za mtandao wa facebook,unaomiliki Instagram,You Tube pamoja na programu ya moja kwa moja ya Twitter ya Periscope ,Instagram imezindua programu mpya inayoruhusu wateja wake kuweka matangazo ya moja kwa moja wakati wowote.
Mtu yeyote anayetazama anaweza kutoa maoni yake kwa kuweka emoji ambazo hujitokeza katika video hiyo ya moja kwa moja.
Inaonekana kuwa ya kawaida,lakini kuna tofauti kubwa.Mara tu unapomaliza kuweka matangazo yako hupotea kabisa.
Hiyo inamaanisha hutaweza tena kusambaza link ya video yako kwa wanaotazama na hawataweza kuiona tena baada ya matangazo hayo.
Katika taarifa, msemaji wa Instagram alisema kuwa hiyo inalenga kuwafanya wateja kuhisi faraja na kuweza kusambaza chochote wanachotaka kusambaza.
Programu hiyo itasambazwa kwa kundi la wateja wa mtandao huo kabla ya kutumika na kila mtu katika kipindi cha wiki chache zijazo.

JUSTIN BIEBER AONEKANA AKIMPIGA NGUMI SHABIKI.

Image result for JUSTIN BIEBER
JUSTIN BIEBER.
Bado mwanamziki Bieber anaendelea na mikasa yake ya kupigana hadharani. Kanda ya video inayomuonesha Justin Bieber akimpiga ngumi shabiki wake usoni imetolewa.
Mtu huyo anaonekana kupeleka mkono wake katika dirisha la gari ya Bieber ambapo anapigwa ngumi na kuachwa akitoka damu mdomoni.
Kanda hiyo inaonekana kurekodiwa mjini Barcelona,ambapo msanii huyo alikuwa akitumbuiza ikiwa ni miongoni mwa ziara yake ya muziki.
Gari moja linaendeshwa polepole katika umati wa watu na msani huyo wa miaka 22 anaonekana kuwa katika kiti cha nyuma huku kioo chake cha dirisha la gari kikiwa wazi.
Shabiki huyo anaonekana kuingiza mkono katika dirisha la gari hilo na kujaribu kumshika Bieber.Wakati gari linapoondoka mkono unaonekana ukitoka katika dirisha hilo.
Shabiki huyo baadaye anarudi nyuma na kuisogelea kamera akiwa na damu katika meno yake na midomo.
Newsbeat imewasiliana na wawakilishi wa msanii huyo lakini haijapata tamko lolote kutoka kwao.
Mapema siku hiyo msanii huyo alipigwa picha akifanya zoezi na wachezaji wa Barcelona.

AL QAEDA YATHIBITISHA KUUAWA KWA KIONGOZI WAO MKUBWA.

Ndege za kivita za Marekani zilimlenga al-Qahtani katika mji wa Kunar
Kundi la kigaidi la Al-Qaeda limethibitisha kuuawa kwa kiongozi wao mkubwa Farouq al-Qahtani huko kaskazini Mashariki mwa Afghanistan katika mapigano na vikosi vya marekani mwezi mmoja uliopita.
Huko mjini Washington wamethibitisha kifo hicho kutokea November 15 yalikuwa ni makabiliano adhimu.
Lakini Al-Qaeda wamesema kuwa mkewe na watoto waliuwawa pia japo hawakujulikana kijeshi.
Vikosi vya Marekani vimeiweka Al-Qahtani mzaliwa wa Saudi huko Quatar kama mtu wanayemtafuta sana kwao akituhumiwa kuhusika na mipango ya mashambulizi huko Marekani na Ulaya.