Wakazi wa Kiluvya Mailimoja hadi Tamko Kibaha waliojenga ndani ya hifadhi ya barabara ya Morogoro wametakiwa kubomoa majengo yao kabla ya bomoabomoa kuanza Novemba 24.
Bomoabomoa hiyo itawahusu wakazi ambao majengo yao yapo ndani ya mita 60 kila upande wa barabara na ambao tayari nyumba zao zimeekewa alama ya X kuwataarifu kuwa wamejenga sehemu sio sahihi.
Mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo alisema katika kikao cha bodi ya barabara kuwa wananchi watambue kuwa taarifa walizopewa za kubomolewa nyumba zao ni za kweli na itahusisha nyumba zote zilizo ndani ya mita 60 kila upande na sio 120 kama ilivyosemwa awali.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumta Mshama alisema "mimi bado naona tunawasumbua hawa wananchi wakati hawana tabu ya kuondoka. Wote waliowekewa X wanajua siku yoyote wanatakiwa kuondoka".
Tuesday, September 13, 2016
KIBAHA KUKUMBWA NA BOMOABOMOA NOVEMBA.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment