Tuesday, September 13, 2016

VITAMBULISHO VYA TAIFA KUBADILISHWA.

Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa (NIDA) inatarajia kubadilisha vitambulisho vyote vya zamani ambavyo havina saini, huku ikitarajia kutoa vitambulisho vipya vyenye saini kwa wananchi wote waliokamilisha taratibu za usajili na utambuzi kwa kuchukuliwa alama ya kibayologia ikiwemo alama za vidole, picha na saini ya kielektroniki.

Aidha inatarajia kutoa vitambulisho vipya kuanzia Septemba 14 katika ofisi zote za NIDA za wilaya. Taarifa iliyotolewa jana Dar es salaam na Kaimu mkurugenzi mkuu wa NIDA Andrew Massawe alisema kwa sasa vitambulisho vya zamani vitaendelea kutumika pamoja na vipya huku taratibu za kubadilisha zikiendelea.


No comments: