Tamasha la Nyama Choma linafanyika leo katika viwanja vya Leaders Club kuanzia saa Sita mchana, kwa kiingilio cha shilingi 10,000 huku msanii wa Afrika Kusini DJ Maphorisa ataburudisha katika tamasha hilo.
TAZAMA ALIVYOWASILI AIRPORT.
Tamasha la Nyama Choma linafanyika leo katika viwanja vya Leaders Club kuanzia saa Sita mchana, kwa kiingilio cha shilingi 10,000 huku msanii wa Afrika Kusini DJ Maphorisa ataburudisha katika tamasha hilo.
TAZAMA ALIVYOWASILI AIRPORT.
Kiongozi wa kundi la Mkubwa na wanawe, Mkubwa Fella siku ya jana aliwaita vyombo mbalimbali vya habari kuonyesha nyumba wanayoishi vijana wa kundi la YA MOTO BAND .
Mkubwa Fella amechukua hatua hiyo kwa sababu watu walikuwa wakisema Ya Moto wanaishi kwenye vibanda, sasa ameamua kuwaonyesha na kudhihirisha kuwa yasemwayo siyo ya kweli.
TAZAMA PICHA ZA NYUMBA YA "YA MOTO BAND" HAPA CHINI.
Muigizaji katika tasnia ya Bongo Movie Shamsa Ford (Chausiku), hatimaye adhihirisha watu na wasanii wenzake kwa kufunga pingu za maisha na mfanyabiashara maarufu mjini anayejulikana kama Chiddy Mapenzi.
TAZAMA PICHA ZAO ZA HARUSI.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli amewataka wananchi wa Pemba wasibabaishwe na wanasiasa waliofilisika, wanaowadanganya watu na kusisitiza kuwa uchaguzi mkuu umekwisha na hautafanyika mwingine hadi 2020 na Ali Mohammed Shein ndio Rais halali wa Zanzibar.
Amewakemea wanasiasa wanaopita kila kona na wakitembea Ulaya, amesema safari zao hizo zitaishia vichochoroni kwani Rais aliyepo madarakani kwa sasa ni Dk.Shein.
"Nataka niwaambie hao wanaokwenda nje kwa kujitangaza na kujitapa, kwamba Rais aliyepo madarakani kwa sasa ni Dk. Shein...uchaguzi umekwisha na utafanyika mwingine ifikapo 2020" alisema Rais Magufuli.
Rais Magufuli alisema hayo wakati akihutubia wananchi wa mikoa miwili, kisiwa cha Pemba ya kaskazini na kusini katika mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Gombani ya kale, uliokuwa na lengo la kutoa shukrani kwa wananchi wa Pemba kwa kumpigia kura katika uchaguzi wa Oktoba mwaka Jana.
Alisema anakerwa na matukio ya vitendo vya chuki na uhasama ikiwemo watu kuchomeana mali zao ikiwemo mikarafuu, neema ambayo wananchi wamepewa na Mungu.
Alisema matukio hayo yanafanywa kwa lengo la kujenga chuki na uhasama huku baadhi ya watu wakiathirika vibaya baada ya kuharibiwa mazao yao.
Aliongeza kuwa, wakati akila kiapo cha utii na uaminifu aliahidi kulinda Muungano pamoja na amani na utulivu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo kuwaonya viongozi wanaopandikiza chuki na uhasama kwamba atapambana nao kwa nguvu zote.
Aliviagiza vyombo vya ulinzi kuhakikisha vinawasaka watu wote wanaofanya vurugu kiasi kuhatarisha amani na utulivu.
"Mimi nawashangaa sana watu wa Pemba, mmepata Rais mpole sana ambaye anatoka Pemba, sasa sijui mnataka nini jamani" alihoji Magufuli.
Dk.Magufuli alisema tangu kumalizika kwa marudio ya uchaguzi mkuu Machi mwaka huu, viongozi wa vyama vya upinzani hasa Chama cha Wananchi (CUF) waliosusia uchaguzi huo ambao Dk. Shein alishinda kwa kishindo kwa asilimia 91.4 wamekuwa wakipita ndani na nje ya nchi wakidai uchaguzi huo haukua halali.
Mhe.Waziri Jenista Mhagama.
Taasisi za fedha na benki zimeombwa kuwa na dirisha la wajasiriamali wadogo, badala ya kuwajumuisha na wajasiriamali wakubwa.
Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, kazi, Vijana, Ajira na wenye ulemavu, Jenista Muhagama alisema hatua hiyo itasaidia wajasiriamali wadogo kujikomboa kiuchumi na kupata mikopo yenye masharti nafuu ili kuendeleza biashara zao.
Mhagama alisema hayo alipofunga kongamano la huduma za kifedha na uwezeshaji, jijini Dar es salaam.
"Taasisi za fedha na mabenki muwe na dirisha la wajasiriamali wadogo ili kuwasaidia kujikomboa kiuchumi na kupata mikopo yenye masharti nafuu ili kuendeleza biashara zao. Msiwajumuishe wajasiriamali wadogo na wakubwa" alisema Mhagama kwenye kongamano hilo ambapo wajasiriamali walipata mafunzo na jinsi ya kupata huduma za kifedha kutoka kwenye benki na taasisi za kifedha.
"Mliosimamia kongamano hili muanzishe kanzidata ili iwe rahisi kuwapata wajasiriamali pale walipo. Tuanzishe ushirikiano kati ya New brand, Vicoba na serikali na vyombo vya fedha. Zipo fursa za kupata mikopo mfano, kanzidata itawawezesha wale waliopata elimu ya ujasiriamali kuongeza uchumi wao na kuongeza nafasi za ajira" alisema Mhagama.
Serikali Mkoa wa Dodoma imesema Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa atahamia rasmi mkoa huo baada ya vikao vya Bunge kumalizika vinavyoanza wiki ijayo Septemba 6.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana, alisema baada ya kufika Dodoma ataanza kuratibu utaratibu wa Wizara mbalimbali kuanza kuhamia Makao Makuu hayo ya nchi.
Pamoja na hiyo jeshi la polisi limejipanga kuongeza vituo vya polisi ili kuimarisha ulinzi wakati serikali itakapohamia na hakuna mwananchi atakayenyang'anywa ardhi yake kwa sababu yoyote ile.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana, Rugimbana alisema kama mkoa walishauri ujio huo ufanyike Mara baada ya vikao vya Bunge na Waziri Mkuu ameridhia swala hilo.
Alisema Waziri Mkuu atakuwa mratibu wa Wizara zote kuhamia Dodoma na kazi hiyo ataianza rasmi mara baada ya kuwasili mkoani humo.
Alisema maandalizi yanaendelea vizuri na ukarabati wa nyumba ya Waziri umefikia asilimia 90.
Alisema Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Christine Mndeme aliyekutana na makundi mbalimbali kwa ajili ya mapokezi ya Waziri Mkuu.
"Awali tulisema atakuja Septemba mosi lakini baada ya kushauriana tumeona aje mara baada ya vikao vya Bunge kwani pilikapilika nyingi zitakuwa zimepungua, kama serikali ikiamua kuja leo tutaipokea kwani maandalizi ya serikali kuja Dodoma yamekamilika kwa asilimia 70" alisema Christine.
Mwelekezi na mwigizaji mashuhuri wa filamu Jackie Chan atapokea tuzo ya staha ya Oscar kwa mchango wake mkubwa katika tasnia ya filamu.
Jopo linalotoa tuzo za Oscar pia limeidhinisha kutunzwa kwa mhariri Anne Coates, mwelekezi Lynn Stalmaster na mwandalizi wa filamu za makala Frederick Wiseman.
Rais wa jopo hilo Cherly Boone Isaacs amewataja wanne hao kama waasisi halisi na stadi katika kazi walioifanya.
Chan (62), alikuwa muigizaji nyota katika filamu nyingi za Kung fu zilizoandaliwa katika nchi yake ya kuzaliwa Hong Kong.
Alivuma kimataifa kwa filamu kama vile Rumble in the bronx, Rush hour na filamu ya vibonzo ya Kung fu panda.