Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) umetangaza kusitisha maandamano waliyokuwa wamepanga kufanya ili kuunga mkono juhudi na kazi inayofanywa na Rais Magufuli, ikielezwa ni kutokana na kutii katazo la jeshi la polisi nchini.
Umesema kuwa umepokea majibu ya barua yao kutoka kwa mkuu wa jeshi la polisi (IGP) Ernest Mangu inayowataka kuacha kufanya maandamano yao kwa sababu polisi wamezuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa na maandamano nchi nzima.
Taarifa iliyotolewa na Kaimu Katibu mkuu wake Shaka Hamdu Shaka, alisema mbali na barua hiyo pia wamefikia uamuzi huo unatokana na utii, nidhamu na kizingatia utaratibu wa mamlaka za juu ndani ya chama.
Wednesday, August 31, 2016
UVCCM KUSITISHA MAANDAMANO YA AMANI WALIYOPANGA KUFANYA SEPTEMBA MOSI.
Tuesday, August 30, 2016
MAANDAMANO YA UKUTA MARUFUKU KUFANYIKA DODOMA.
Jeshi la polisi mkoani Dodoma limepiga marufuku na kuwataka wananchi wasishiriki katika maandamano yatakayofanyika Septemba mosi.
Limesema maandamano hayo ya ukuta ambayo yameandaliwa na Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA si halali na yana nia ya kupotosha na kuvuruga amani ya nchi.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari leo, Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma Lazaro Mambosasa amesema kwa muda mrefu kumekuwa na makundi ya wafuasi wa Chadema kuhamasishana ili kufanya vurugu kupitia hoja ya maandamano waliyoyapa jina la UKUTA.
"Wapo watu wanaosambaza machapisho mbalimbali yenye kauli za uchochezi katika fulana, mabango na katika mitandao ya kijamii na pia wapo wanaofanya kampeni zisizo halali nyumba kwa nyumba kuwashawishi watu kufanya uhalifu huo" alisema kamanda.
WALIOJIHUSISHA NA WATUMISHI HEWA MATATANI.
Serikali imeanza kuwashughulikia wale wote waliojihusisha na fedha za watumishi hewa ambapo hadi sasa watumishi 839 wapo katika hatua mbalimbali wakiwemo waliofikishwa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) na wengine wanaendelea kuhojiwa na polisi kwa ajili ya kufikishwa mahakamani.
Sambamba na hilo, serikali unatarajia kutoa ajira mpya 71,496 kwa mwaka huu wa fedha baada ya kuwaondoa wafanyakazi hewa.
Waziri wa nchi, ofisi ya Rais (Utumishi na utawala bora), Angellah Kairuki aliyasema hayo wakati akizungumzia utekelezaji wa mipango na mikakati ya Wizara yake katika kipindi cha "tunatekeleza" kinachorushwa na televisheni ya TBC1.
"Kwa sasa wapo watumishi wanahojiwa na kuchukuliwa maelezo yao polisi na upelelezi utakapokamilika watachukuliwa hatua za kisheria" alisema.
LEMA AWAGOMEA POLISI.
Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema, amezua tafrani kwenye mahakama ya hakimu mkazi Arusha baada ya askari polisi waliomleta awali kutaka apande gari kwenda mahabusu kwa sababu ya kutokidhi masharti ya dhamana. Awali Lema, alisomewa makosa mawili yaliyokuwa yakimkabili mbele ya Hakimu mkazi wa mahakama hiyo, Desdery Kamugisha na Wakili wa serikali Innocent Njau. Katika mashtaka ya kwanza ni la kutuma ujumbe mfupi wa maneno kutoka kwake kwenda kwa Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo. Mashtaka ya pili kutumia Whatsapp kwa ajili ya kuwashawishi wananchi wa jiji la Arusha kuandamana Septemba Mosi. Baada ya Lema kusomewa mashtaka hayo, Hakimu Kamugisha alimuuliza kama ni kweli au la, na Lema alikana baada ya kukana Wakili Njau aliomba Lema asipewe dhamana kwa sababu wana taarifa za kiintelijensia kuwa, endapo atapewa dhamana maisha yake yatakuwa matatani. Hoja ya Wakili huyo wa serikali, ilipingwa na wakili wa utetezi John Mallya. Baada ya mabishano hayo Hakimu Kamugisha alitupilia mbali pingamizi la Wakili Njau la Lema kunyimwa dhamana. Baada ya sharti la dhamana kutolewa, wadhamini wawili walijitokeza ambao ni madiwani wa jiji la Arusha, lakini hali tofauti ilijitokeza baada ya wakili wa serikali Njau kukagua barua ya kumdhamini Lema na kugundua kuna kasoro za matumizi ya majina. Kutokana na sintofahamu hiyo wakili alikubaliana na hoja ya Njau na kusema kuwa Lema atafute wadhamini wengine na kuahirisha kesi hiyo kwa muda hadi Septemba 19 mwaka huu. Baada ya kusomewa kesi hiyo, ikasomwa kesi ya pili ambayo inadaiwa ya kutoa lugha ya uchochezi kati ya Agosti mosi hadi 26 mwaka huu kwa njia ya kurekodi kwa sauti "audio clip" na kurusha kwenye mitandao ya kijamii kwa ajili ya kuhamasisha maandamano Septemba mosi mwaka huu. Saa 8:20 mchana mapolisi walimtoa mahabusu na kumpandisha kwenye gari wakitaka kumpeleka mahabusu Kisongo. Kutokana na sintofahamu hiyo Lema alibishana na polisi hao huku akiwa na Mawakili wake, Mallya na James Lyatuu walihoji kuwa wanampeleka wapi wakati muda wa mahakama haujafika. "Muda wa mahakama haujafika mnanipeleka wapi, nasema nitafia hapa mahakamani muda huu ni saa nane, muda wa mahakama haujaisha mnanipeleka wapi, siendi, mniue, siendi popote mniue hapahapa, muda wa mahakama haujaisha bro, mnanipeleka wapi na kwanini mnanifanyia hivyo, nasema siendi kokote bora kufa, sikubali" alisema Lema.
Monday, August 29, 2016
KAMPUNI YA MBOWE IMEBAKIZA SIKU MOJA KULIPA BIL.1.3/-NHC.
Kampuni ya Mbowe Hotels Limited (MHL) imebakiza siku ya leo tu, kuwa tayari imelipa deni la shilingi Bilioni 1.3 ya kodi ambayo inadaiwa na shirika la nyumba la Taifa (NHC) ili kujinasua katika hatari ya kuondolewa katika jengo la shirika hilo lililopo katika makutano ya mitaa ya Mkwepu na Indira Ghadhi Makunganya jijini Dar es salaam.
Jengo hilo ni maarufu kutokana na kuendesha shughuli mbalimbali za starehe na burudani kutokana na kuwepo kwa Club maarufu ya Billcanas.
Hatua hiyo inatokana na notisi mbili zilizotolewa; Moja na shirika la nyumba la Taifa Juni 24, mwaka huu ikitishia kuvunja makubaliano ya mkataba wa ukodishaji wa jengo hilo na kufuatia na notisi ya kampuni ya udalali ya mahakama ya fosters, ambazo zote zinakamilisha muda wake leo.
Kampuni hiyo inamilikiwa na mwenyekiti wa taifa wa Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe.
Mbowe alinukuliwa na vyombo vya habari mwishoni mwa wiki akilihusisha deni hilo na masuala ya kisiasa, kwa madai kuwa suala hilo linakuzwa na kupotoshwa ili kumnyamazisha katika harakati za kisiasa, bila kukiri uwepo wa shauri baina ya pande hizo mbili juu ya deni hilo.
Mkurugenzi mkuu wa NHC Nehemiah Mchechu, alithibitisha kuwepo kwa mpango wa kuiondoa kwa nguvu kampuni ya Mbowe katika jengo hilo.
"Ni kweli kuwa tumempa mpangaji wetu huyo Mbowe notisi ya kumuondoa. Kampuni ya Hoteli za Mbowe ni miongoni mwa wateja wetu watatu ambao ni wadaiwa sugu wa kodi ya pango kwa wateja binafsi nchini" alisema.
Mchechu alisema suala hilo ni la kibiashara na halina mahusiano na masuala ya siasa, kama ilivyodaiwa na Mbowe hivi karibuni alipoongea na vyombo vya habari.
"NHC haina uhusiano na masuala ya kisiasa wala kujihusisha nayo, hatuna uhusiano wowote na masuala ya umoja wa kupambana na udikteta (UKUTA), namuomba Mbowe atambue kuwa hili ni suala la kibiashara na si vinginevyo" alisema Mchechu.
Hatua ya NHC ya kuandika notisi ya kuvunja mkataba, ilitokana na kampuni ya Mbowe kushindwa kujibu na kusaini hati mpya ya makubaliano ya namna ya ukodishaji wa jengo hilo uliowasilishwa kwa kampuni hiyo January 18, 2015.
LIST YA WALIOCHUKUA TUZO ZA MTV VIDEO MUSIC AWARDS.
Tuzo za MTV VMAs zilifanyika jana huko Marekani na wafuatao ni wasanii waliochukua tuzo hizo huku mwanadada Beyonce akiongoza kwa kuchukua tuzo 8;
VIDEO OF THE YEAR - Formation (Beyonce).
BEST MALE VIDEO - This is what you came for (Calvin Harris ft Rihanna).
BEST FEMALE VIDEO - Hold up (Beyonce).
BEST POP VIDEO - Formation (Beyonce).
BEST HIP HOP VIDEO - Hotline bring (Drake).
BEST ROCK VIDEO - Heathens (Twenty one pilots).
BEST ELECTRONIC VIDEO - How deep is your love (Calvin Harris & Discipline).
BEST COLLABORATION VIDEO - Work from home (Fifth harmony ft Ty Dolla $ign).
BEST NEW ARTIST - D.N.C.E
BEST BREAKTHROUGH LONGFORM VIDEO - Lemonade (Beyonce).
BEST DIRECTION - Formation (Beyonce).
BEST VISUAL EFFECTS - Up & up (Cold play).
BEST ART DIRECTION - Black star (David Bowie).
BEST EDITING - Formation (Beyonce).
BEST CINEMATOGRAPHY - Formation (Beyonce).
BEST CHOREOGRAPHY - Formation (Beyonce).
SONG OF SUMMER - All in my head (flex) (Fifth harmony).
YANGA YANG'ARA TENA.
Mabingwa watetezi wa ligi kuu bara, yanga jana kuanza vizuri kampeni zao kwa ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Afrikan Lyon katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa taifa Dar es salaam.
Yanga imeanza kutetea taji lake baada ya kutupwa nje ya michuano ya kimataifa ya kombe la shirikisho Afrika kwa kufungwa na TP mazembe ya Congo DR mabao 3-1 katika mechi ya mwisho ya makundi.
Ikicheza soka safi Yanga ilichukua dakika 19 kuandika bao la kuongoza lililofungwa na Deus Kaseke baada ya kuunganisha pasi safi ya Simon Msuva.
Afrikan Lyon ambayo ni mechi ya kwanza ilitoka sare 1-1 na mechi ya Azam, jana ilizidiwa karibu kila idara na kuonekana kuchoka hasa katika kipindi cha pili.
Msuva aliiandikia Yanga bao la pili katika dakika ya 59 akiunganisha pasi ya Haruna Niyonzima kabla ya kumpiga chenga kipa wa Lyon na kuujaza mpira wavuni.
Pamoja na kuelemewa huko, Lyon walijitahidi kufanya mashambulizi ambapo katika dakika ya 76 Tito Okello alishindwa kumalizia krosi akiwa amebaki peke yake na kipa.
Yanga iliendeleza mashambulizi na dakika ya 90 Amisi Tambwe alikosa bao baada ya mpira wa kichwa aliopiga kugonga mwamba na mpira kurudi uwanjani.
Zikiwa zimebaki sekunde chache mpira kumalizika, Juma Mahadhi aliyeingia uwanjani kuchukua nafasi ya Msuva aliandika bao la tatu kwa Yanga baaa ya kazi nzuri ya Niyonzima.
Yanga itacheza mechi ya pili keshokutwa ambapo itaminyana na JKT Ruvu kwenye uwanja huo huo wa Taifa.
Kutoka kwenye uwanja wa CCM kirumba Mwanza, Alexander Sanga anaripoti kuwa wenyeji Toto Africans wameshindwa kuutumia vizuri uwanja wa nyumbani baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Mbeya city.
Wageni Mbeya City waliandika bao hilo katika dakika ya tano lililofungwa na Haruna Shamte kwa mpira wa adhabu uliokwenda moja kwa moja golini.