Wednesday, November 2, 2016
WALIOHUSIKA NA KIFO CHA MASHALI WASAKWA.
MBUNGE AKAMATWA NA BUNDUKI 11.
LADY JAY DEE KIZIMBANI.
Tuesday, November 1, 2016
FARAJA NYARANDU AHAMASISHA WATANZANIA KUACHA KUMSEMA VIBAYA MISS TANZANIA 2016.
Aliyewahi kuwa Miss Tanzania, Faraja Nyalandu amemkingia kifua mshindi wa mwaka huu Diana Edward akisema hata yeye aliposhinda alizushiwa mambo mengi, lakini anashukuru kwa kuwa yalimjenga.
Katika waraka wake wenye maneno 223 aliouweka kwenye mtandao wa Instagram, mrembo huyo alisema alikaribishwa katika dunia ya umaarufu kwa kashfa lakini kwa msaada wazazi wake alifanikiwa kusimamia malengo yake.
Alimtaka Miss Tanzania afanye anachokiamini na kupuuzia maneno ya watu kwa sababu yanaweza kumtoa katika njia yake.
“Njia ya mafanikio ni ngumu, kwako Miss Tanzania wetu fanya kile unachokiamini, usikubali maneno haya ya watu yakuondoe katika mstari, kwa Watanzania wenzangu tujitahidi kuyaunga mkono yaliyo mazuri, tusibomoe…Tujenge,” alisema.
Akizungumzia ushindi wake, Diana alisema amejipanga kulitumikia vyema hasa kukomesha vitendo vya ukeketaji katika jamii ya Kimasai.
MWANAFUNZI ALIGONGA GARI LA POLISI KWA SABABU YA KUJIPIGA SELFIE.
TANZANIA KUSHIRIKI MASHINDANO INDIA.
UTAFITI:SUMU YA NYOKA NI DAWA YA KUMALIZA UCHUNGU.
Joka mwenye sumu kali zaidi duniani huenda akawa jibu la kupatikana dawa ya kupunguza uchungu. Hii ni kwa mujibu ya wanasayansi.
Joka anayejulikana kama 'Blue Coral' ndiye mwenye sumu kali zaidi na hupatikana zaizi Kusini Mashariki mwa Bara Asia. Utafiti mpya uliochapishwa kwenye jarida la afya la Toxin umepata joka huyo huwalenga maadui wake ambao husababisha uchungu kwa binadamu.
Wanasayansi wanasema huenda sumu hii ikatumika kutengeneza dawa ya uchungu. Baadhi ya wanyama ambao sumu yao imetumika kutengeneza dawa ni pamoja na konokono wa baharini na bui bui wa sumu.
Wanasayansi sasa wanataka joka huyu kuhifadhiwa hususan baada ya maeneo mengi anakopatikana kugeuzwa kuwa mashamba ya michikichi. Wanasayansi walifanya utafiti wao katika nchi za China, Singapore na Marekani.
Watafiti wanasema japo kwa mwanadamu nyoka huwa adui, lakini wakati huu huenda akawa suluhu la matatizo mengi ya kiafya.