Wakati mwili wa bondia Thomas Mashali ukitarajiwa kuzikwa leo, watu wanne wanasakwa na polisi wakituhumiwa kuhusika na kifo chake.
Ndugu wa Mashali, Emmanuel Mashali akiwa nyumbani kwao, Tandale kwa Mtogole, Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam alisema kwamba ndugu yao ataagwa leo saa 7:00 mchana na kuzikwa jioni kwenye makaburi ya Kinondoni.
“Tunajaribu kuomba kutumia Viwanja vya Leaders Club kufanya shughuli za kuaga, kama itashindika shughuli hiyo itafanyika kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Tandale,” alisema Emmanuel na kuongeza: “Shughuli ya kuaga mwili itaanza saa 7:00 mchana na saa 10:00 jioni tutamuhifadhi ndugu yetu kwenye makaburi ya Kinondoni.”
Akizungumzia kifo hicho, Emmanuel alisema taarifa za awali walizopata ni kwamba bondia huyo alipigwa na watu kadhaa baada ya kumpigia yowe za mwizi.
No comments:
Post a Comment