Saturday, August 27, 2016

LEMA AKAMATWA ARUSHA KWA KOSA LA UCHOCHEZI.

Mhe. Godbless Lema

Mbunge wa jimbo la Arusha mjini, Godbless Lema amesekwa rumande na jeshi la polisi mkoani Arusha kwa kosa la kusambaza maneno ya uchochezi katika mitandao ya kijamii, usiku wa kuamkia jana.

Lema alikamatwa na polisi, alfajiri nyumbani kwake kata ya Engutoto, Njiro ndani ya jiji la Arusha akiwa bado hajaamka.

Kamanda wa polisi wa mkoa, Charles Mkumbo alikiri Polisi kumsweka rumande mbunge huyo na kusema kuwa inamhoji na kufahamu ni kwa nini alisambaza maneno ya kichochezi yenye lengo la kuvunja amani ya nchi. Alisema Lema alikamatwa nyumbani kwake Alfajiri akiwa amelala.

Alisema baadhi ya maneno hayo ni "kama mauti imepoteza utukufu wake hakuna statement ya kurudisha nyuma Arusha kuandamana".

Kwa mujibu wa kamanda, maneno hayo aliyoyatoa Lema ni ya uchochezi na kuvuruga amani ya nchi na ndiyo maana wanamshikiria kwa mahojiano juu ya kauli zake hizo.

Alisema Watanzania wanatambua umuhimu wa amani na hakuna mtu aliye juu ya sheria, hivyo ni vyema wakaheshimu utulivu uliopo.


POLISI NA MAJAMBAZI WAJIBISHANA KWA RISASI HUKO MKURANGA.

Majibizano ya risasi baina ya polisi na majambazi yaliyodumu kwa takribani saa saba   kuanzia saa 8:20 usiku wa kuamkia jana mtaa wa Vikindu Mashariki, Mkuranga mkoani pwani, yamesababisha vifo vya watu wawili akiwemo askari polisi na mtu mwingine anayedhaniwa kuwa ni miongoni mwa majambazi.

Mbali ya milio ya risasi, mtaa huo pia ulitanda moshi kutokana na mabomu ya machozi yaliyopigwa mfululizo na kuibua taharuki kubwa kwa wakazi wake. Mmoja wa majirani katika nyumba iliyozingiwa waliyoishi watuhumiwa, Mjenge Faki alisema walishtuka usingizini na kuanza kusikia milipuko ya risasi na ghafla wakaanza kutokwa na machozi kufuatia hewa hiyo ya machozi kuanza kusambaa.

Katika majibizano hayo, askari aliyekuwa katika majibizano na mtuhumiwa walikufa hapo hapo. Hata hivyo kamanda wa polisi mkoani Pwani, Boniventure Mushongi, licha la kuwepo eneo la tukio, hakuwa tayari kuzungumzia lolote, akisema mwenye jukumu la kuzungumzia tukio hilo ni Kamanda wa polisi kanda ya Dar es salaam, Simon Sirro.

Naye Kamanda Sirro akizungumzia hilo alisema, taarifa rasmi ya tukio hilo zitatokewa leo kwani bado wanakusanya taarifa kuhusiana na tukio hilo. Lakini Mkuu wa mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo alisema katika mapambano hayo, Jeshi la polisi limepoteza askari mmoja, lakini bado lipo imara na litaendelea kuwasaka wahalifu popote watakapokuwepo.

"Askari wetu katika shughuri zake za kupambana na majambazi ameuawa hapa leo (Jana) usiku, ni tukio baya katika mkoa wetu, wilaya yetu na nchi yetu kwa ujumla. Hawa ni wahalifu, lakini mbaya zaidi hata watoto na familia zao zinaaminika wana mafunzo maalumu ya kulinda wazazi wao ambao ni wahalifu" alisema Ndikilo.

Aliongeza kuwa, kama waalifu hao walidhani kwa kuua askari watakuwa wametimiza malengo yao, basi wamechelewa kwani watawawinda popote pale watakapokwenda. Kwa mujibu wa Faki milio ya risasi na mabomu ilisikika katika nyumba inayosadikiwa kumilikiwa na mkazi wa Temeke, aliyetajwa kuwa ni Salum Kingungo.

"Tulianza kusikia kama watu wanakimbizana kutoka eneo la juu barabarani na kelele hizo zikaja kuishia ndani ya nyumba hii walianza kusikia majibizano baina ya watu waliokuwa nje na mingine kutoka ndani, lakini hatukuweza kujua kinachoendelea kwani tulijawa na hofu kubwa", alisema Faki.

Alisema alishindwa kutoka nje na hata walipobaini kuwa ni askari, hawakuruhusiwa kutoka nje hadi ilipohitimu saa tano asubuhi.

Katika majibizano hayo ya risasi na mabomu, nyumba inayodaiwa yalikuwa makazi ya watuhumiwa hao, iliharibiwa vibaya. Baada ya hali kutulia, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Ndikilo akiwa na kamati yake ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Pwani, alipata fursa ya kuzungumza na wananchi.

Baada ya kutembelea nyumba hiyo na kujionea hali halisi, waliwataka wananchi wa Mkulanga na mkoa wa Pwani kwa ujumla kuwa watulivu kwani serikali imejipanga na kupambana na watu wachache ambao sio waaminifu.


Friday, August 26, 2016

J LO NA CASPER SMART WAVUNJA MAHUSIANO YAO.

Casper Smart na J Lo

J Lo (47) na Casper (29) walianza mahusiano yao oktoba 2011, ilisemekana kama waliachana mwaka 2014 ila wachunguzi walisema hawakugombana na walikuwa wakiishi nyumba moja.

Wiki kadhaa zilizopita walikuwa vizuri tu hadi J Lo akampaisha aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Marc Antony katika tamasha lake huko Las Vegas.

Hicho ndo kinasemekana ndio chanzo cha J Lo na Casper kuvunja mahusiano yao na kila mtu kuendelea na shughuri zake kama apo awali.


JARIDA LA FORBES LIMEMTAJA THE ROCK KAMA MSANII WA KWANZA DUNIANI ANAYELIPWA KIASI KIKUBWA CHA PESA.

The Rock

Muigizaji maarufu wa Marekani na Canada,  Dwayne Douglas Johnson maarufu kama "The Rock" ametajwa katika jarida la Forbes kama ni msanii namba moja duniani anayelipwa pesa kubwa kiasi cha dola za kimarekani $64.5 milioni kwa mwaka.

Hayo mamilioni yametokana na kulipwa kwenye movie alizocheza kama Central Intelligence na Fast 8 na pia movie ambayo bado haijatoka inayoitwa Baywatch.

Juhudi alizoonyesha kwenye movie ya Fast and furious na movie yake ya San Andreas ya mwaka 2015 zimezaa matunda hayo.


MUOGELEAJI WA MAREKANI RYAN LOTCHE ASHITAKIWA.

Polisi nchini Brazil wamemshtaki muogeleaji wa olmpiki wa Marekani Ryan Lotche kwa kutoa madai ya uongo kuwa yeye na wenzake watatu waliibiwa kwa kushikiwa bunduki wakati wa michuano ya Rio, kitu ambacho ni upotoshaji.

Uhalifu huo hukumu yake ni miezi nane jela.

Msemaji wa polisi ameeleza kuwa kesi hiyo imepelekwa mahakamani na Lotche atatakiwa kujibu mashtaka hayo. Idara ya Marekani  imesema inatambua ombi hilo.

Lotche ameondoka Brazil kabla hajaojiwa na polisi. Ameomba msamaha kwa kusema uongo juu ya kuibiwa. Lotche amepoteza wadhamini wake wakubwa wanne kufuatia tukio hilo na hivyo kuweka hatarini kazi yake ya uogeleaji.


SAMATTA ASAIDIA KLABU YAKE KUFUZU MASHINDANO YA EUROPA LEAGUE.

Mchezaji wa kimataifa kutoka Tanzania Mbwana Ally Samatta amepata nafasi ya kucheza hatua ya makundi ligi ndogo ya klabu Ulaya, Europa League.

Hii ni baada ya klabu yake KRC Genk ya Ubelgiji kupata ushindi wa jumla 4-2 mechi ya kufuzu hatua ya makundi dhidi ya wapinzani wao Lokomotiva Zagreb ya Croatia.

Genk walipata ushindi wa 2-0 mechi iliyochezwa jana jioni.

Klabu hizo mbili zilitoka sare 2-2 mechi ya mkondo wa kwanza.

Samatta alifungia klabu yake bao la kwanza dakika ya pili naye mwenzake Leon Bailey akafunga la pili muda mfupi baada ya mapumziko.

Samatta pia alioneshwa kadi ya njano dakika ya 69.

Droo ya hatua ya makundi itafanywa mjini Monaco baadae leo ijumaa mwendo wa saa tisa za Afrika Mashariki.


WANASAYANSI WAGUNDUA SAYARI INAYOFANANA NA DUNIA.

Wanasayansi wamegundua sayari ambao inakaribiana sana na dunia kwa mazingira na ukubwa wake ambayo inazunguka nyota ijulikanayo kama Proxima Centauri iliyo na mfumo unaokaribia zaidi mfumo wetu wa jua.

Sayari hiyo ambayo kwa sasa imepewa jina la Proxima b inazunguka nyota hiyo katika eneo ambalo kuna uwezo mkubwa sana wa kupatikana kwa maji.

Proxima inapatikana umbali wa kilomita tirioni 40 na inaweza kumchukua mtu akitumia teknologia ya sasa ya vyombo vya usafiri wa anga za juu, maelfu ya miaka kufika huko juu.

Licha ya kwamba ni mbali sana kugunduliwa kwa sayari hiyo, huenda kukasisimua hisia na mawazo ya binadamu na wanasayansi kuhusu kuwepo kwa viumbe katika sayari nyingine au uwezekano wa wakati mmoja watu kuishi kwenye sayari nyingine.

"Kusema ukweli kufika huko kwa sasa hiyo ni kama hadithi ya kubuni kisayansi, lakini watu sasa wanalifikiria hilo na si jambo lisiloweza kufikirika kwamba wakati mmoja mtu anaweza kutuma chombo huko.