Tuesday, October 25, 2016

MAJINA YA WACHEZAJI WANAOWANIA TUZO ZA FIFA BALLON d'Or 2016.


Image result for ballon d'or 2016 image
  1. Sergio Aguero (Manchester City)
  2. Pierre-Emerick Aubameyang (Borussia Dortmund)
  3. Gareth Bale (Real Madrid)
  4. Gianluigi Buffon (Juventus)
  5. Cristiano Ronaldo (Real Madrid)
  6. Kevin de Bruyne (Manchester City)
  7. Paulo Dybala (Juventus)
  8. Diego Godin (Atletico Madrid)
  9. Antoine Griezmann (Atletico Madrid)
  10. Gonzalo Higuain (Juventus)
  11. Zlatan Ibrahimovic (Manchester United)
  12. Andres Iniesta (Barcelona)
  13. Koke (Atletico Madrid)
  14. Toni Kroos (Real Madrid)
  15. Robert Lewandowski (Bayern Munich)
  16. Hugo Lloris (Tottenham Hotspur)
  17. Riyad Mahrez (Leicester City)
  18. Lionel Messi (Barcelona)
  19. Luka Modric (Real Madrid)
  20. Thomas Muller (Bayern Munich)
  21. Manuel Neuer (Bayern Munich)
  22. Neymar (Barcelona)
  23. Dimitri Payet (West Ham)
  24. Pepe (Real Madrid)
  25. Paul Pogba (Manchester United)
  26. Rui Patricio (Sporting Lisbon)
  27. Sergio Ramos (Real Madrid)
  28. Luis Suarez (Barcelona)
  29. Jamie Vardy (Leicester City)
  30. Arturo Vidal (Bayern Munich).

Tuzo hiyo hutolewa na Ufaransa kila mwaka tangu mwaka 1956, lakini kwa kipindi cha miaka sita iliopita tuzo hiyo ilibadilika na kuwa Fifa Ballon d'Or kwa ushirikiano na shirikisho la soka duniani Fifa.
Mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi alishinda tuzo hiyo mwaka uliopita kwa mara ya tano .

MTOTO MCHANGA AZALIWA MARA MBILI

Lynlee, dadazake na mama yao Margaret Hawkins Boemer

Mtoto mchanga wa kike kutoka Lewisville, Texas, 'amezaliwa' mara mbili baada ya kutolewa katika kizazi cha mamake kwa dakika 20 ili kufanyiwa upasuaji.
Akiwa miezi minne mja mzito, Margaret Hawkins Boemer aligundua kuwa binti yake, Lynlee Hope, ana uvimbe katika uti wake wa mgongo.
Uvimbe huo unoajulikana kama sacrococcygeal teratoma, ulikuwa unasukuma damu kutoka kwa mtoto huo - jambo lililoongeza hatari ya moyo wa mtoto huyo kutofanya kazi.
Baby Lynlee alikuwana uzito wa chini ya kilo moja wakati wapasuaji walipomtoa kwenye uzao wa mamake.
Bi Boemer awali alikuwa amebeba mimba ya pacha, lakini alimpoteza mtoto mmoja kabla ya kumaliza miezi mitatu ya kwanza. Awali alishauriwa kuitoa mimba hiyo kabla ya madakatari wa wa hospitali ya watoto ya Texas Children's Fetal Center kumpndekezea upasuaji huo wa hatari.
Uzito wa uvimbe huo na ule wa mtoto ulikuwa karibu sawa wakati upasuaji ulipofanywa. Aliarifiwa kuwa mwanawe Lynlee ana asilimia 50 ya kufanikiwa kuishi.
Bi Boemer aliambia CNN: " nikiwa na miezi mitano, uvimbe huo ulikuwa unasitisha moyo wake kufanya kazi, kwahivyo ilikuwa ni uamuzi baina ya kuruhusu uvimbe huo ummalize au kumpa nafasi ya kuishi.
"Ulikuwa uamuzi wa rahisi kwetu: Tulikuwa tunataka kumpa maisha."
'Moyo wake ulisiti kupiga'.
Lynlee Boemer alitolewa kutoka uzao wa mamake kufanyiwa upasuaji ili kuokoa maisha yake.. kabla ya miezi mitatu baadaye kuzaliwa kupitia upasuaji.

Upasuaji

Daktari Darrell Cass wa Texas Children's Fetal Centre nimojawapo ya matabibu waliotekeleza upasuaji huo. Amesema uvimbe huo ulikuwa mkubwa, kiasi cha kuhitaji upasuaji mkubwa kuufikia, jambo lililohatarisha maisha ya mtoto huyo.
Moyo wa Lynlee nusra usite kupiga wakati wa upasuaji huo lakini mtaalamu wa moyo alimsaidia kuendelea kuishi wakati uvimbe huo ulipakuwa unatolea, aliongeza.
Madaktari hao baadaye walimrudisha katika uzao wa mamake na kuufunga uzao kwa kuushona.
Bi Boemer alisalia kitandani kwa wiki 12 zilizofuata, na Lynlee alizaliwa kwa mara ya pili mnamo Juni 6.
Alizaliwa kwa upasuaji akiwa aribu kutumiza miezi tisa tumbano, na alikuwa na karibu kilo mbili na nusu.
Lynlee alipofikisha siku nane baada ya kuzaliwa, alifanyiwa upasuaji mwingine kutoa uvimbe uliosalia katika uti wake wa mgongo.
Dr Cass anasema mtoto huyo sasa amerudi nyumbani na anaendelea vizuri.
"Bado ni mchanga lakini anaendelea vizuri," amethibitisha.
Sacrococcygeal teratoma ni uvimbe usiojitokeza sana na huwapata watoto 30,000 kati ya 70,000 wanaozaliwa.
Haijulikani husababishwa na nini lakini watoto wa kike huathirika mara nne zaidi kuliko wavulana.

BETRI ZINAZOTUMIWA KATIKA SIMU ZINA SUMU.

Betri za Lithium-ion zinazodaiwa kuwa na sumuZaidi ya gesi 100 zinazoweza kusababisha kifo hutolewa na betri zinazopatikana miongoni mwa mabilioni ya vifaa vinavyotumiwa na raia wengi duniani kama vile simu aina ya smartphone na vipatakilishi kulingana na utafiti mpya.
Utafiti huo ulibaini gesi 100 zenye sumu zinazotolewa na betri za Lithium, ikiwemo ile ya kaboni monoksaidi, ambayo inaweza kusababisha kujikuna katika ngozi, macho na pua mbali na kuathiri mazingira.
Watafiti kutoka taasisi ya ulinzi ya NBC nchini Marekani pamoja na chuo kikuu cha Tsinghua nchini China wamesema kuwa watu wengi huenda hawajui hatari ya betri kupata moto, kuharibika ama kutumia chaji isiofaa katika vifaa hivyo, jarida la Science Explorer limeripoti.
Katika utafiti huo mpya,walichunguza betri moja ya kuchaji inayojulikana kama Lithium-ion,ambayo huwekwa katika vifaa vinavyotumika kila mwaka.
''Siku hizi,Betri za Lithium-ion hukuzwa na serikali nyingi duniani kama kawi inayopatikana kwa haraka ili kuviwasha vifaa vyote ikiwemo magari ya kielektroniki hadi simu," alisema Jie Sun, profesa mkuu katika taasisi ya ulinzi ya NBC.
Sun na wenzake waligundua sababu kadhaa ambazo zinaweza kuongeza gesi zenye sumu zinazotolewa.
Betri zilizopata chaji zaidi hutoa gesi zaidi za sumu ikilinganishwa na betri ilio na asilimia 50 ya chaji.

GARI LILILOIBIWA LIKIWA NA MTOTO LAPATIKANA BAGAMOYO.

Hatimaye gari liloibwa likiwa na mtoto ndani la Ofisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Innocent Dallu, limepatikana Bagamoyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Bonventura Mushongi aliwataja waliokamatwa na gari hilo kuwa ni Ezekiel Daudi (25), mfanyabiashara na mkazi wa Moshi aliyekuwa kwenye gari hilo huku aliyekuwa anaendesha Joshua Eliya Adam akitoroka. Daudi analisaida Jeshi la Polisi kuhusu tukio hilo.
Mtego uliowekwa na Jeshi la Polisi katika barabara ya Bagamoyo-Msata, Kata ya Kiwangwa juzi usiku uliwezesha kunaswa kwa wezi pamoja na gari waliloiba.
Watu hao waliiba gari aina ya Toyota Harrier T400DEH mali ya ofisa afya wa JWTZ ambaye alikuwa akifanya kazi katika Hospitali ya Lugalo na kwa sasa amehamishiwa Darfur nchini Sudan ingawa sasa yuko mapumzikoni jijini Dar es Salaam.
Wakati gari linaibwa ndani kulikuwa na watoto wawili, lakini walimshusha mmoja wa kiume Phillip na kuondoka na mwingine wa kike mwenye umri wa miaka mitatu, Lightness Dallu.

KOCHA PLUIJM AONDOLEWA YANGA.

Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Pluijm amesema ahofii lolote hata kama mabosi wake wameleta kocha mpya atakuwa tayari kuondoka.
Jana kwenye gazeti moja la michezo iliripotiwa kuwasili kwa kocha mpya Mzambia George Lwandamina ambaye anadaiwa kuletwa na Kampuni ya Yanga Yetu iliyoikodisha klabu ya Yanga.
Kwa zaidi ya mwezi sasa kumekuwa na tetesi za Yanga kubadili benchi la ufundi kwa madai ya kutoridhishwa na mwenendo wa timu kwa sasa.
Yanga iko nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 21 nyuma ya Simba inayoongoza kwa pointi 29.
Hata hivyo chini ya Pluijm, Yanga ilitwaa ubingwa wa Ligi Kuu misimu miwili mfululizo na kucheza hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika. Kocha huyo ambaye kwa sasa ana mkataba na Zesco ya Zambia, anadaiwa kuja kufanya mazungumzo ya mwisho na Yanga kabla ya kurudi tena Zambia kuweka mambo sawa na kisha kurudi rasmi kuwafundisha mabingwa hao wa soka Tanzania bara.
Akizungumza jana na gazeti hili, Pluijm alikiri kusikia taarifa za ujio wa kocha mpya kwenye vyombo vya habari. “Sina taarifa zozote kutoka kwa viongozi wala Mwenyekiti (Yusuf Manji), lakini sina wasiwasi na lolote kama watakuwa wamefikia uamuzi huo, nitakuwa tayari kuondoka, maisha lazima yaendelee,” alisema Pluijm ambaye amekuwa kipenzi cha mashabiki wa Yanga.
Alipoulizwa kuhusu hilo, Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit alisema hakuna taarifa yoyote ya ujio wa kocha mpya na kama kuna lolote kuhusu benchi lao la ufundi uongozi utatangaza rasmi.
“Suala la kocha bado hatuwezi kuingia mkataba na kocha mpya wakati Pluijm bado ana mkataba, lakini kama kuna chochote tutaweka wazi tu,” alisema.
Pluijm anakumbwa na dhahama hiyo ikiwa ametoka kuongeza mkataba wa miaka miwili kuifundisha timu hiyo mwanzoni mwa msimu huu.

SERIKALI ZA MITAA ZAONGOZA KWA RUSHWA.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki ameitaja Mamlaka ya Serikali za Mitaa kuwa ndio inayoongoza kwa vitendo vya rushwa kisekta nchini, kutokana na kuwa na majalada mengi ya kesi za rushwa zinazoendelea mahakamani.
Aidha, amebainisha kuwa Mahakama ya Ufisadi iko mbioni kuanza kazi, baada ya Jaji Mkuu kukamilisha kutengeneza kanuni za uendeshaji pamoja na mafunzo kwa majaji.
Akizungumza katika kikao kati ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali ya Mtaa mjini Dodoma jana, Kairuki alisema kwa mujibu wa mchanganuo wa kesi zilizopo mahakamani kisekta kuanzia Juni mwaka huu, zinaonesha mamlaka hiyo na sekta ya afya ndio zinaongoza kwa kuhusishwa na vitendo vya rushwa.
Alisema mchanganuo huo unaonesha kuwa hadi Juni mwaka huu, kesi zilizopo mahakamani za kisekta ni 509 na kati ya hizo kesi 209 sawa na asilimia 41 zinaihusu Serikali za Mitaa na kufuatiwa na sekta ya afya ambayo ina kesi 63 sawa na asilimia 12.
“Sekta hii pia kwa mwaka 2015/16 imeonekana kuongoza kwa kuwa na majalada mengi yanayohusu tuhuma za rushwa. Kati ya majalada 3,082 yanayoendelea na uchunguzi, majalada 1,357 sawa na asilimia 44 yanahusu mamlaka hii,” alisisitiza.
Alisema serikali inaendelea kuchukua hatua katika kuzuia na kupambana na rushwa katika eneo hilo hilo la mamlaka ya serikali za mitaa kutokana na kuongoza kwa kuwa na tuhuma na kesi nyingi za rushwa zinazoendelea mahakamani.
Kuhusu hatua za kuanzishwa kwa Mahakama ya Ufisadi zilipofikia, Kairuki alisema mahakama hiyo ipo mbioni kuanza kazi na mashauri yake yatachukua muda wa miezi tisa kusikilizwa na kutolewa maamuzi.
“Jaji Mkuu ameshamaliza kuandaa kanuni na majaji wameshapewa mafunzo na maelekezo kwamba ndani ya miezi tisa shauri ziwe zimekamilika,” alisema.
Kuhusu utendaji wa taasisi ya Takukuru, waziri huyo alisema kwa kipindi cha mwaka 2015/16 kesi mpya 424 zilifunguliwa katika mahakama mbalimbali nchini ikiwa ni ongezeko la kesi 110 ikilinganishwa na mwaka 2014/15.
Pia alifafanua kuwa kati ya kesi hizo, kesi 177 zilihusu kifungu cha 15 cha sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa sura ya 329 na kesi 247 zilihusu vifungu vingine, ambavyo mashitaka dhidi ya watuhumiwa mahakamani yanahitaji kibali cha Mkurugenzi wa Mashitaka ya Umma na katika kesi hizo kesi kubwa zilizokuwa 15. Pia alisema Takukuru imefanikiwa kuokoa Sh 43.78 ikiwa ni ongezeko la Sh 36.78 bilioni ziliozookolewa mwaka 2014/15.
Alisema fedha hizo zilitokana na kitendo cha taasisi hiyo kuanzisha kitengo cha ufuatiliaji wa fedha na mali za watuhumiwa zilizopatikana kwa njia ya rushwa kwa kutaifishwa kwa mali za watuhumiwa.
Kwa upande wa wajumbe wa kamati hiyo walibainisha kuwa adhabu inayotolewa kwa watu wanaotiwa hatiani kwa vitendo vya rushwa haiendani na kosa wanalolitenda.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jasson Rweikiza aliishauri serikali kuchukua hatua za kudhibiti tatizo la rushwa kwa kuwaboreshea maslahi watendaji wadogo ili kuondokana na rushwa ndogondogo.
Alisema serikali inatakiwa iweke mikakati ya kudhibiti rushwa kuanzia ngazi za chini ikiwemo kuingiza somo la rushwa katika mitaala ya shule.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kitengo cha Uchunguzi wa Takukuru, Alex Mfungo alifafanua kuwa upelelezi wa kesi za rushwa, umekuwa ukichelewa kwa sababu wanataka kujiridhisha kwanza kabla ya kupeleka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

KIKWETE: UDSM IPEWE TUZO YA HESHIMA.


                                                                                          JAKAYA MRISHO KIKWETE      .
Dar es Salaam. Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Jakaya Kikwete amependekeza chuo hicho kupewa tuzo ya heshima baada ya kutoa wahitimu walio na mchango katika nyanja mbalimbali nchini, akiwamo Rais John Magufuli na Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa.
Kikwete amesema hayo jana alipokuwa akifungua maadhimisho ya miaka 55, tangu kuanzishwa  kwa  chuo hicho.
 “Chuo hiki kilianza na wanafunzi 14 kikiwa maeneo ya Lumumba ila kwa sasa tunahudumia wanafunzi 24,000 kutoka ndani na nje ya nchi, hii ni hatua kubwa, kimeleta mchango mkubwa sana kwa taifa,” amesema.