Tuesday, January 24, 2017

MPIGIE KURA JIHAN KWENYE MASHINDANO YA MISS UNIVERSE.


"VOTE! VOTE! VOTE!!The door is open
sasa tunaweza kumpigia kura mrembo wetu @jihandimack
Kwakutumia Applications tulizopakua na kama bado hujapakua basi waweza pakua sasa na umpigie kura @jihandimack
kutoka Tanzania.

Jinsi ya kumpigia kura Jihan katika mashindano ya Miss Universe kuanzia tarehe 23 January 2017:


1) VODI: Pakua Vodi app katika Google Store au Apple Store
2) Kupitia tovuti ya www.missuniverse.com
3) MISS U APP: Pakua Miss U app
4) TWITTER: Tweet kwa kutumia hashtag #MissUniverse alafu utatumia hashtag maalum ya Jihan itakayotolewa muda si mrefu. 


Upigaji kura utakapoanza kila mtu ataweza kupiga kura mara 10 kwa siku kwa kila akaunti aliyoisajili.

Kumbuka kuwa website ya missuniverse.com ni mtandao pekee ambapo upigaji kura utaendeshwa

Saturday, January 21, 2017

ALICHOKIANDIA FARAJA NYARANDU INSTAGRAM KUHUSU MELANIA TRUMP.


Mwaka 1996, Melanija Knavs akiwa na miaka 26 aliingia Marekani akiwa na ndoto ya kuwa mwanamitindo. Jana, akiwa ni Melania Trump, alishika Biblia aliyotumia kuapa Rais wa 45 wa Marekani, Rais Donald Trump.


Ukiniuliza kama alidhani kuna siku angesimama Capitol Hill kwenye uapisho wa Rais kama Mke wa Rais wa Marekani, nitakwambia hapana. Lakini ndivyo Mungu alivyo. Leo hii huhitaji kumheshimu Melania Trump, ila utaheshimu mamlaka yake, na kwakuwa amekalia hicho kiti chenye mamlaka, utajikuta unamheshimu tu.


Unaweza kudhihaki historia yake, lafudhi yake au hata kazi aliyokuwa anafanya. Ila Mungu keshampa kibali cha kuwa hapo. Hata huyo Askari ukute alimpigia kura Hillary ila anajikuta akitii mamlaka ya Melania.


Kiongozi anaweza akatoka sehemu chakavu isiyo na tumaini. Chini, mwisho kabisa. Kumbuka hata Bwana Yesu alizaliwa katika zizi la ng'ombe. Mungu anaweza kumuinua mtu usiyemtarajia na kumfanya mtawala wako. 


Mungu anaweza kukuinua wewe usiyejidhania na kukuweka mahali pa juu. Mipango Yake si kama yetu. Usidharau mtu yeyote na muhimu Usijidharau. Njia Zake si kama zetu.

Friday, January 20, 2017

TAMASHA KUBWA LA DIAMOND PLATNUMZ KUFANYIKA UWANJA WA TAIFA.

Image result for SALAAM SK
SALLAM SK.

Meneja wa Diamond Platnumz, fundi mitambo Sallam SK ametangaza ujio mpya wa tamasha kubwa la Diamonds Are Forever 2017 ambapo safari hii litafanyikia katika uwanja wa Taifa.

Muimbaji huyo alifanya tamasha hilo kwa mara ya kwanza nchini mwaka 2012 katika ukumbi wa Mlimani City show ambayo ilihudhuriwa na watu wengi kwa kiingilio cha Tsh 50,000.
.
Sallam alizungumza live na mashabiki katika mtandao wa Instagram (Insta Live) alisema show hiyo ipo kwenye maandalizi na itafanyika uwanja wa Taifa.
.

“Mjiandae na Diamonds Are Forever 2017, Diamonds Are Forever 2017 is back,” alisema

Meneja huyo alidai safari hii tamasha hilo litafanyika uwanja wa taifa ili kuwapa fursa watu wengi zaidi ya kuudhuria.

QUEEN DARLEEN: SIJAWAHI KUTONGOZWA.

Image result for QUEEN DARLEEN
QUEEN DARLEEN.
Msanii kutoka WCB, Queen Darleen amefunguka jana usiku katika kipindi cha Pillow talk kinachorushwa na Times Fm kuwa, hajawahi kutongozwa.

Queen alisema''kusema ukweli mimi sijawahi kutongozwa na mwanaume, kwa asilimia kubwa mimi ndio huwa nawtongoza wanaume.

SHAMSA FORD: WASANII WENGI HAWAOLEWI KWA SABABU WANATAKA WANAUME WENYE HELA.

Image result for SHAMSA FORD
SHAMSA FORD.
Leo katika kipindi cha Leo Tena kinachorushwa na radio stesheni ya Clouds FM, msanii wa kike maarufu kama Shamsa Ford alifunguka na kuhusiana na sanaa yake na mahusiano yake.

Shamsa Ford alisema baada ya ndoa heshima kwa mumewe anayefahamika kwa jina la Chiddy Mapenzi iliongezeka na akaanza kumuogopa, kwa sababu kabla hajaolewa alikuwa anamchukulia poa tu.

Pia Shamsa alisema kuwa wasanii wengi wa kike wa bongo hawaolewi kwa sababu wanataka mwanaume ambaye amekamilika kwa kila kitu, wakati mwanaume anatengenezwa na mwanamke mwenyewe.

Shamsa alimaliza kwa kuwataja wasanii wa bongo movie anaowakubali ni Gabo na Rihama.

WASANII WATAKAO TUMBUIZA KWENYE SHEREHE ZA KUAPISHWA KWA TRUMP SIKU YA LEO.

Jackie Evancho
JACKIE EVANCHO.
Heshima ya kuongoza wimbo wa taifa imepewa msichana wa umri wa miaka 16, Jackie Evancho, ambaye alimaliza wa pili katika shindano la America's Got Talent mwaka 2010.
Sam Moore
SAM NA DAVE.
Sam Moore, wa bendi ya watu wawili ya Sam and Dave, ataongoza wakati wa dansi rasmi ya Liberty and Freedom (Uhuru).
The Rockettes
RADIO CITY ROCKETTES.
Radio City Rockettes pia watatumbuiza katika dansi hizo rasmi, ingawa hatua hiyo ilipingwa na baadhi ya wanachama wa bendi hiyo.
Wengine watakaotumbuiza katika dansi hizo ni Tim Rushlow na bendi yake ya Big Band, Silhouettes, Pelican212, The Piano Guys, Circus 1903, Cache Olson, Lexi Walker na Erin Boheme.
PIA KUTAKUWA NA DANSI ZA WANAOMPINGA TRUMP. Kutakuwa na dansi mbadala - ambazo zinaitwa Dansi za Amani - ambazo zimeandaliwa na wanaharakati watetezi wa uhuru. Miongoni mwa watakaotumbuiza huko ni dadake Beyonce, Solange Knowles.
Solange Knowles
SOLANGE KNOWLES.
Mwanamuziki wa jazz mshindi wa tuzo ya Esperanza Spalding pia atatumbuiza katika Dansi ya Amani mjini Washington.
Esperanza Spalding

KANYE WEST NI RAFIKI TU WA TRUMP LAKINI HATOTUMBUIZA KATIKA KUAPISHWA KWA RAIS HUYO.

Donald Trump na Kanye West
TRUMP NA KANYE WEST.
Kanye West hatatumbuiza wakati wa sherehe ya kuapishwa kwa rais wa 45 wa Marekani, Donald Trump, waandalizi wa sherehe hiyo wamesema.

Kumekuwa na uvumi kwamba tangu nyota huyo wa muziki alipowaambia watu kwamba angempigia Bw Trump kura iwapo angeshiriki uchaguzi, na kisha wakakutana Trump Tower, basi angekuwa mmoja wa wasanii ambao wangetumbuiza Ijumaa.

Lakini Tom Barrack, mwenyekiti wa kamati andalizi ya sherehe ya kuapishwa kwa rais, alisema kwamba sherehe hiyo si "ukumbi ufaao" kwa West.

Alisema mwanamuziki huyo wa mtindo wa rap ni "jamaa mzuri" lakini "hatujamuomba atumbuize."

Bw Barrack alisema: "Yeye hujichukulia kama rafiki wa rais mteule, lakini huu sio ukumbi wake.

"Ukumbi ambao tunao, upande wa watumbuizaji, umejaa, uko sawa, utakuwa kimsingi wa nyimbo za kitamaduni za Marekani, na Kanye ni jamaa mzuri lakini hatujamuomba atumbuize. Tunaendelea na ajenda yetu."